June 10, 2013



Perez
Rais wa Real Madrid, Florentino Perez amekata mzizi wa fitina na habari za tetesi baada ya kusisitiza kwa mara nyingine kwamba Cristiano Ronaldo hatakwenda Manchester United au timu nyingine yoyote.

Perez amewaambia waandishi mjini Madrid leo kwamba Ronaldo hatahama kwenda Manchester United wala timu nyingine.


“Nafikiri tufunge mjadala wa Ronaldo, maana hatahama, Manchester wanalijua hili na sasa wanaendelea na mambo mengine.

“Sisi tunaanza mipango ya mambo mengine, hivyo Ronaldo bado yupo nasi, pia analijua hilo,” alisema.

Kauli hiyo ya Perez inakata kabisa kiu ya mashabiki wa Man United waliokuwa wanatamani Ronaldo arudi katika klabu hiyo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic