June 17, 2013



 
Kocha wa zamani wa Simba, Talib Hilal hivi karibuni alifanya mafunzo ya mchezo wa soka la ufukweni katika nchi ya Guam.

Talib aliyewahi kuipa Simba ubingwa mwaka 2008, aliongoza mafunzo hayo kwa lengo la kuboresha mchezo huo unaochipukia kwa kasi.


Kocha huyo ambaye sasa ni kocha wa timu ya taifa ya Oman pamoja na mkufunzi wa Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa) amekuwa akifanya mafunzo katika nchi mbalimbali duniani.


“Nimemaliza na Guam, jamaa wamepata faida na nchi yao ni sawa na mkoa mmoja tu kama Morogoro. Lakini sisi nyumbani (Tanzania) bado tumelala na hakuna anayeonyesha kuchangamka,” alisema.

Mwezi uliopita, Hilal alifanya mafunzo kama hayo nchini Uganda ambayo imepania kuanza kucheza Beach Soccer.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic