June 10, 2013



 
WAKIPATA MAELEKEZO KUTOKA KWA MMOJA WA WALIMU WAO AITWAYE ADIRAN::
Na Saleh Ally, Freiburg
Vijana wa Kitanzania walio katika mafunzo ya soka na maisha leo wameibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya timu ya Schallstadt.

Schallstadt moja ya timu inayosifika kwa kuzalisha wachezaji nyota ilijikuta katika wakati mgumu kutoka kwa vijana hao wa Kitanzania.

Mabao ya Watanzania hao wa kikosi kinachofanya mafunzo chini ya Fels Project yalifungwa na Miraji Athumani au Sheva na Carlos Sekule.


Wakati Carlos Protus, Rajab Rashid na Emily Josiah Mgeta wakifanya kazi ya uhakika katika safu ya ulinzi na kumfanya kipa wao apumzike kama yuko pikniki.

Vijana  hao wanaendelea na mafunzo ya soka pamoja na maisha ya kawaida lengo likiwa ni kuwawezesha kuwa imara na uhakika wa kufanya vizuri kama watapata timu za kucheza barani Ulaya, Afrika au kwingineo lakini pia katika maisha ya kila siku.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic