July 16, 2013

OGBU (KULIA) AKIWA KAZINI NA TIMU YAKE YA HEARTLAND....
Kocha Mkuu wa Yanga, Ernie Brandts amesema atampanga mshambuliaji  Brendan Ogbu kutoka Nigeria katika mechi dhidi ya Wanigeria.

Alhamisi, Yanga itacheza mechi ya kirafiki dhidi ya Pillars FC ya Nigeria ambayo inaundwa na wachezaji kutoka timu mbalimbali. Mechi itapigwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar.

Ogbu ni mshambuliaji wa Heartland ya Nigeria ambayo ni moja ya timu kubwa nchini humo na amekuwa tishio kwa upachikaji mabao kwa misimu miwili iliyopita.

Brandts amesema  Ogbu ili apate nafasi ya kumuona na mechi ya pili itakuwa ni ile dhidi ya URA  ya Uganda itakayochezwa Jumapili kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar.


“Kwanza ataanza mazoezi na sisi Jumatano, halafu Alhamisi nitampa nafasi katika mechi ya kirafiki. Lakini baadaye nitampa nafasi tena Jumapili tutakapocheza na timu ya Uganda.

“Bado ni mchezaji ambaye anatakiwa kuangalia, hivyo ningeshauri benchi la ufundi tupewe nafasi kwanza,” alisema.


Mnigeria huyo ametua usiku wa kuamkia leo tayari kufanya majaribio ya kujiunga na Yanga.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic