Ushindi wa mabao 3-0 walioupata Brazil dhidi ya Hispania katika mechi ya fainali ya Kombe la Mabara kwenye Uwanja wa Maraccana jijini Rio, umekuwa ni rekodi mpya dhidi ya Mabingwa hao wa Dunia.
Kwanza, ushindi huo umewafanya wabebe kombe hilo kwamara ya nne, safari hii ikiwa ni mara ya kwanza nyumbani.
Lakini kikubwa zaidi, Hispania
hawakuwahi kufungwa katika fainali tatu, kuanzia fainali ya mwaka Ulaya 2008,
ikashinda bao 1-0 dhidi ya Ujerumani. Ikashinda 1-0 tena kwenye Kombe la Dunia
mwaka 2010 dhidi ya Uholanzi na ushindi wa mabao 4-0 kwenye fainali nyingine ya
Euro dhidi ya Italia mwaka 2012.
0 COMMENTS:
Post a Comment