July 17, 2013



OKWI AKIITUMIKIA ETOILE DU SAHEL (PICHA: ESS, RUHUSA KWA SALEHJEMBE BLOG)


Klabu ya Etoile Du Sahel umeitaka Simba kufanya mchakato wa kumuuza mshambuliaji Emmanuel Okwi ili iweze kurejesha gharama zake za dola 300,000 (zaidi ya Sh milioni 480) inazodai.

Uamuzi huo wa Etoile Du Sahel umetokana na tabia ya Okwi kuchelewa kurejea kazini kila anapopewa nafasi ya kwenda kuitumikia timu yake ya taifa ‘The Cranes’.

Katibu Mkuu wa Etoile Du Sahel, Adel Gith amesema kuwa wamejitahidi kadiri ya uwezo wao lakini inaonekana mchezaji huyo ni tatizo katika suala la nidhamu na hawezi kupata soko sehemu yoyote duniani hasa kwa watu makini.


“Inawezekana kuna sehemu nyingi ambayo alikuwa anatakiwa kabla ya kuja hapa, Simba wanaweza kuwa wanajua ndiyo maana baada ya kuja hapa tuliwaambia kuwa wamuuze halafu wachukue fedha yao,” alisema.

“Lakini wao walisisitiza kuwa wanataka fedha ingawa walituambia wakisikia anatakiwa sehemu, basi watatusaidia. Lakini inaonekana hapa hatakuwa na nafasi, hawezi kuwa mchezaji anayekaa nje timu kwa zaidi ya wiki bila ya taarifa na hapokezi simu za viongozi,” alisema.

Taarifa kutoka ndani ya Simba zinaeleza uongozi wa Msimbazi ulisisitiza kuwa hauhusiki na suala la kuuzwa, kwanza ni fedha wanazodai na biashara nyingine ifuatie.

“Unajua alikwenda Katibu Mkuu (Evodius) Mtawala na Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili (Zacharia) Hans Pope. Wao walisisitiza kwamba wanachotaka ni fedha kwanza, suala la kusaidiana kumuuza litafuatia,” alisema.

Kwa upande wa uongozi wa Simba, Mtawala alisema wanachojua wanawadai Etoile Du Sahel, wanachotaka ni kulipwa fedha zao tu.
“Kwanza kabisa ni fedha, kama watashindwa tutalifikisha hili suala Fifa. 

Biashara ya kumuuza Okwi si kazi yetu kwa kuwa ni mchezaji wao,” alisema Mtawala huku akisisitiza Simba sasa haiko katika nafasi ya kulizungumzia kwa urefu suala hilo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic