July 17, 2013

KAZIMOTO (KUSHOTO) AKIWA MAZOEZINI SIMBA..
Siku moja baada ya kutoweka katika kambi ya timu ya taifa, imebainika kiungo nyota wa Simba, Mwinyi Kazimoto ametimkia nchini Qatar.
Awali kulikuwa na tetesi huenda Kazimoto amekimbilia nchini humo lakini rafiki yake wa karibu ambaye pia ni mchezaji amethibitisha.

“Kweli amesema anakwenda Qatar, mipango imeishakamilika nay eye amekwenda kujaribu bahati,” alisema na alipoulizwa kwa nini hakuaga.
“Aliogopa, si unaona (Shomari) Kapombe leo yuko hapa, alipata nafasi ya kwenda Uholanzi lakini TFF ikamzuia na sasa yupo tu.

“Mwinyi akaona mambo kama ya Kapombe yanaweza kumkuta, kaamua aondoke na kwenda kujaribu bahati,” alisema rafiki yake huyo.
Taarifa zinaeleza Kazimoto ameondoka usiku wa leo, saa tatu usiku na ndege ya Qatar Airways kwenda nchini humo kujiunga na timu ambayo bado haijajulikana.


“Hiyo timu imemuambia aende na yenye itajua namna ya kumalizana na Simba,” kilisisitiza chanzo.

Lakini mchana wa leo, TFF imesisitiza lazima itatoa adhabu kwa Kazimoto ambayo itakuwa ni kufungiwa kutokana na utovu wa nidhamu wa kutoroka katika kambi ya timu ya taifa.

Kazimoto alitoroka wakati Stars inaondoka Dar es Salaam kwenda Mwanza kuweka kambi kujiandaa kuivaa Uganda katika mechi ya marudiano kuwania kucheza fainali za Chan.

Hali hiyo ilisababisha Kocha Kim Poulsen amrejeshe kiungo kinda Mudathiri Yahaya ambaye alimuacha katika kikosi kilichokwenda Mwanza kwenda kuweka kambi.


Kama atafungiwa kucheza, huenda ikamtia ugumu Kazimoto kucheza katika timu aliyokwenda Qatar hata kama Simba watakuwa wamekubali.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic