July 16, 2013



...Lulu

 Kampuni ya Wananchi Group kupitia huduma yake ya Zuku, imetoa zawadi ya tuzo na fedha kwa wasanii wa filamu za Kiswahili zilizoshinda kwenye Tamasha la Filamu la Kimataifa Zanzibar (Ziff).

Wasanii hao akiwemo Elizabeth Michael maarufu kama Lulu walikabidhiwa zawadi hizo mbele ya waandishi wa habari kwenye ofisi za Zuku, Morocco jijini Dar es Salaam.
 
Jacq akizungumza, kulia ni bosi wa Zuku, Fadhili Mwaseba


Mwenyekiti wa kampuni hiyo, Ali Mafuruki aliwataja washindi wa tuzo hizo kuwa ni Lulu aliyeshinda tuzo ya Msanii Bora wa Kike kupitia filamu yake ya Woman of Principle.

Halafu Bond Bin Suleiman aliyetwaa tuzo tatu, Muigizaji Bora, Muongozaji Bora na Mtunzi Bora.
 
....Bin Suleiman

...Amir Shivji

Mwingine ni Amir Shivji ambaye filamu yake ya Shoe Shine iliyoongoza kupendwa wengi. Tuzo hizo zilienda sambamba na kitita cha shilingi laki tano kila moja.

Mafuruki aliwataka wananchi kujipatia ving’amuzi vya Zuku kwa bei nafuu ambapo wataweza kuona chaneli zaidi ya 85 zenye muonekano mzuri bila kusahau chaneli ya filamu za Kiswahili.

Zuku ina ving’amuzi vya aina mbalimbali ambavyo vimekuwa vikipendwa na watu wengi zaidi kutokana na kuwa na chaneli bora za filamu, michezo, muziki, habari.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic