July 16, 2013



 
Masatu akiwa na Saleh Ally
Beki nyota wa zamani wa Simba, George Magere Masatu amerejea nchini baada ya kuishi ughaibuni kwa zaidi ya miaka 10.
Masatu alikuwa kicheza soka la kulipwa nchini Indonesia lakini baadaye akastabu na kuamua kufanya kazi ya ukocha.

Masatu alifanya kazi kwa miaka mitatu na ushee akiwa mwalimu katika kituo cha watoto wadogo kilicho chini ya Arsenal ya England.

Akiwa Indonesia amekuwa akifanya kazi katika kituo hicho kwa kushirikiana na makocha wengine wakiwemo kutoka England, Cameroon pia Indonesia.

Baada ya kucheza soka nchini baadaye Uarabuni, Masatu aliondoka nchini na kwenda Indonesia ambako alicheza soka kwa zaidi ya miaka mitano kabla ya kustaafu na baadaye akapata kazi katika shule ya watoto iliyo chini ya klabu maarufu ya England ya Arsenal ambako alifanya kazi kwa miaka mitatu na ushee.

Masatu anasema sasa amerejea nyumbani Tanzania baada ya kuishi Indonesia kwa zaidi ya miaka nane na atafanya nini?

“Kuna mambo mengi sana ya kufanya, lakini tunaweza kuzungumza kwanza masuala ya soka na baadaye, nitawaeleza mambo yatakavyokuwa na kipi ambacho nimepanga kukifanya,” anasema Masatu katika mahojiano yake ya kwanza na gazeti la Championi ikiwa ni siku moja tu baada ya kutua nchini.

Kesho, Masatu ataelezea kuhusiana na mambo mengi ya maisha yake. Usiache kufuatilia kupitia blog hii ya wanamichezo na wapenda burudani…


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic