August 9, 2013



Straika wa West Ham, Andy Carroll, juzi usiku alionyesha kuwa ni mtu wa kujali watu wengine baada ya kumkabidhi ombaomba pauni 50 ambazo ni zaidi ya shilingi 130,000.

Carroll ambaye alikuwa majeruhi kwa muda, alimpa fedha hiyo ombaomba huyo ambaye alimsogelea karibu wakati alipokuwa ndani ya Jiji la London, England.
 
Msimu uliopita, mshambuliaji huyo alikuwa akichezea timu hiyo kwa mkopo akitokea Liverpool ambapo alishindwa kupata namba kwenye kikosi cha kwanza kutokana na kiwango chake kutokuwa cha kuridhisha. Hatimaye West Ham ikamsajili rasmi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic