August 9, 2013



Kocha wa Chelsea, Jose Mourinho amesisitiza kuwa ataendelea kumuwania mshambuliaji wa Manchester United, Wayne Rooney mpaka sekunde ya mwisho ya usajili wa safari hii.

Rooney amekuwa akitajwa kuwaniwa na Chelsea lakini klabu yake imekataa ofa mbili zilizotolewa na Chelsea inayomuwania kwa nguvu.

Uamuzi wa kocha huyo raia wa Ureno umekuja wakati ambapo Kocha wa Man United, David Moyes akisisitiza kuwa hana mpango wa kumuuza Rooney ambaye ana umri wa miaka 27.

“Tulipeleka ofa na Manchester United wakakataa, tusubiri kitakachotokea, tunafanya mambo kisheria, hatujazungumza na mchezaji kwa kuwa kila kitu kinakwenda kwa utaratibu.

“Tuna washambuliaji wazuri lakini tutaendelea kuwamia mpaka siku ya mwisho,” alisema Mourinho ambaye pia amesisitiza kuwa klabu yake haina mpango wa kumuuza beki David Luiz kwenda Barcelona.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic