August 14, 2013

Kiungo mshambuliaji wa Simba, Amri Kiemba, amesema kikosi chao kipo tayari kwa kuwania ubingwa wa Ligi Kuu Bara msimu wa 2013/2014.

Akizungumza  jijini  Dar es Salaam, Kiemba alisema kikosi chao kipo tayari na mashabiki hawatakiwi kuwa na hofu juu ya hilo na sasa wanapigania kuhakikisha wanatwaa ubingwa.

Alisema licha ya kuwa na matatizo madogomadogo, anaamini kocha atayafanyia kazi na ligi ikianza tu wataona moto wao.



“Timu yetu ipo tayari kushiriki ligi na tutapigana ili kuhakikisha tunatwaa ubingwa kwa kuwa tunashiriki kwa ajili hiyo tu,” alisema Kiemba.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic