August 14, 2013



Uwezekano wa beki Mbuyu Twite kucheza katika mechi ya Ngao ya Jamii dhidi ya Azam FC, Jumamosi ni mdogo sana.

Kocha Mkuu wa Yanga, Ernie Brandts, amesema uwezekano wa beki huyo ni mdogo kutokana na kuwa majeruhi.
 
Timu hizo zinatarajiwa kuvaana Jumamosi ijayo katika mchezo wa Ngao ya Jamii utakaopigwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.


Akizungumza na Championi Jumatano, Brandts alisema beki huyo amekaa nje ya uwanja kwa wiki mbili bila mazoezi, hivyo ni ngumu kwake kutoa maamuzi ya kucheza au kutocheza.

Brandts alisema beki huyo ameanza mazoezi juzi Jumatatu, hivyo ataendelea kuangalia maendeleo yake katika mazoezi ingawa jambo la kucheza kwenye mechi hiyo ni gumu sana.

“Hatima ya Mbuyu ya kucheza au kutocheza katika mechi ya Ngao ya Jamii dhidi ya Azam bado sijaijua.

“Ameanza mazoezi mepesi na wenzake, ni mapema kutangaza kuwa atacheza au hatacheza, ninaendelea kumuangalia kujua kama yupo fiti au vipi,” alisema Brandts.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic