August 9, 2013



Beki Rio Ferdinand ameambiwa hataruhusiwa kutumia mechi ya hisani ya timu yake kwa ajili ya kutangaza nembo ya bidhaa zake kwenye kipute cha timu yake ya Manchester United dhidi ya Seville, leo Ijumaa kwenye Uwanja wa Old Trafford.

Mechi hiyo ambayo itashuhudiwa na zaidi ya mashabiki 50,000 itachezwa kwa ajili yake katika kusherekea kutimia miaka 10 ya uwepo wake klabuni hapo.

Watu wa masoko wa United walikaa kikaa na wale wa upande wa beki huyo ambapo baada ya majadiliano marefu waliamua kuwa Ferdinand, 34, hatakiwi kutumia mechi hiyo kuipromoti nembo ya bidhaa zake binafsi inayotambulika kwa kusomeka kama namba 5 (#5).

Mara kadhaa Rio amekuwa akionekana amevaa fulana, kofia na vingine vikiwa na alama hiyo ambayo inawakilisha biashara zake kadhaa nje ya soka.

Lakini wakati uamuzi huo unafanyika, imeelezwa kuwa umechekewa kwa kuwa kuna vipeperushi na nembo kadha zenye alama ya #5 ambazo nyingi zilikuwa zimeshasambazwa kwa mashabiki.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic