August 10, 2013


Simba wameila vizuri Simba Day baada ya kuwatwanga wageni wao SC Villa ya Uganda kwa mabao 4-1.

SC Villa ndiyo timu iliyomlea kiungo nyota wa zamani wa Simba, Emmanuel Okwi ambaye amejiunga na Etoile du Sahel ya Tunisia.
Katika mechi hiyo, SC Villa ilianza kupata bao katika dakika ya 8 lililofungwa na 8 kupitia kwa Robert Mganga na Jonas Mkude akaisawazishia Simba katika dakika ya 43.



Kipindi cha pili timu hizo zilicheza soka la kasi na kupaniana zaidi lakini Simba walikuwa wenye njaa zaidi ya mabao baada ya kuzitikisa nyavu za SC Villa mara tatu.

Mabao mawili yalifungwa na mshambuliaji wake mpya, Betram Mombeki aliyefunga mawili na Lucian William ‘Gallas’.

KIKOSI CHA SIMBA LEO:
Abel Dhaira, Masoud Nassor ‘Chollo’, Issa Rashid ‘Baba Ubaya’, Joseph Owino, Miraji Adam, Jonas Mkude, Ramadhani Chombo ‘Redondo’, Abdulhalim Humud, Betram Mombeki, Amri Kiemba & Haruna Chanongo.


Kabla ya mechi hiyo, Twalipo walifanikiwa kuwafunga Simba B kwa mabao 6-3.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic