September 27, 2013



 
KAZIMOTO WAKATI AKIWA SIMBA...
Kiungo Mtanzania, Mwinyi Kazimoto amecheza Ligi Daraja la Pili nchini Qatar kwa mara ya kwanza, tena kwa dakika 90, lakini bahati mbaya timu yake ya Al Markhiya imeambulia kipigo cha mabao 2-1.


Akizungumza kutoka jijini Doha, Kazimoto alisema wameanza mechi ya kwanza kwa kipigo lakini wanatarajia kujirekebisha katika mechi nyingine watakayocheza kesho Jumamosi.

“Tumeanza kwa kupoteza, kidogo timu nazisahau majina. Lakini tuna mechi nyingine ya ligi Jumamosi, hii itakuwa ni ya pili. Tuna timu nzuri tu kwa kweli, kuhusiana na kucheza namshukuru Mungu kwa kuwa ninapata nafasi, nimecheza namba nane kwa dakika zote 90 na nilicheza vizuri.

“Kupata namba haikuwa rahisi lakini nimejituma na nitaendelea kufanya hivyo,” alisema Kazimoto alipokuwa ‘akigonga’ stori moja kwa moja na Championi Ijumaa.

Kiungo huyo wa zamani wa Simba alijihakikishia namba wakati wa mechi za kirafiki ambazo aling’ara na kocha wake akaamua kumpa ‘dimba la juu’ ahangaike nalo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic