Beki wa Yanga raia wa Rwanda, Mbuyu
Twite amezidi kuandamwa na mikosi msimu huu, baada ya sasa kubainika wakati
wowote anaweza kufukuzwa katika nyumba aliyopanga kutokana na kushindwa kulipa
kodi.
Taarifa kutoka kwa watu wa karibu na
beki huyo mwenye asili ya DR Congo, ni kuwa yupo katika wakati mgumu kwa kuwa
kodi ambayo alilipiwa na uongozi wa Yanga imeshamalizika na anatakiwa kulipa
tena.
Chanzo cha habari kimeeleza kuwa nyumba
hiyo iliyopo maeneo ya Kinondoni jijini Dar, Mbuyu analipiwa kodi na uongozi wa
klabu hiyo kwa mujibu wa mkataba wake, ambapo kwa mwezi anatakiwa kuilipia Sh
600,000, kodi ambayo inatakiwa kulipwa kwa mwaka mzima.
“Mbuyu ni kama amechanganyikiwa, kama
unakumbuka hivi karibuni aliibiwa mara mbili, lakini sasa hili la kodi limekuja
tena, kibaya zaidi ni tishio la wenye nyumba kutaka kumtimua kama ataendelea
kusumbua kwa malipo, sijajua nini kitaendelea hapa ni jambo la kusubiri,” kilisema
chanzo.
Wakati huohuo, taarifa za uhakika
zinaeleza kuwa mshambuliaji wa Yanga, Didier Kavumbagu naye pia yupo kwenye
hali kama hiyo kwa kuwa kodi ya nyumba anayoishi Mikocheni jijini, imemalizika
na bado haijalipwa.
Mbuyu alipotafutwa alionekana kushtushwa
na taarifa hizo na kusema: “Umeambiwa na nani habari hizo? Tanzania hakuna siri,
kweli nadaiwa kodi ya nyumba naomba ujue hivyo tu na tayari nimeshazungumza na
viongozi wa klabu kulitatua hilo.”
Alipotafutwa Kavumbagu, hakupatikana
mpaka tunaingia mitamboni lakini mmoja wa viongozi alithibitisha hilo na kusema uongozi unalifanyia kazi ndani ya siku chache litakuwa limekamilika.








0 COMMENTS:
Post a Comment