October 7, 2013





Kundi la mashabiki wanaodaiwa kuwa wa Simba, juzi Jumamosi lilitanda nje ya Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam likimsubiri Kocha Msaidizi wa timu hiyo, Jamhuri Kihwelo ‘Julio’ ili kumwambia aondoke katika timu hiyo.


Tukio hilo lilitokea mara baada ya mechi ya Ligi Kuu Tanzania Bara kati ya Simba na Ruvu Shooting kumalizika kwa sare ya bao 1-1.

Blogu hii ilishuhudia kundi hilo la mashabiki likiwa kwenye geti kuu la kuingilia Uwanja wa Taifa, likikagua kila gari iliyokuwa inatoka ili kumnasa Julio.

Mashabiki hao walisikika wakimtuhumu kocha huyo kwamba ndiyo chanzo cha timu yao kufanya vibaya na kuiharibu kwa makusudi.

Kundi hilo la mashabiki lilijaribu kulizunguka gari la waandishi wa Championi na kuomba wamfikishie ujumbe Julio kwamba awaachie Simba yao chini ya Abdallah Kibadeni.

Pia mashabiki walilifuata gari aina ya Mazda Merrina la kiungo mkabaji wa timu hiyo, Abdulhalim Humud wakimsifia na kuhoji sababu ya kuwekwa benchi wakati ana uwezo mkubwa. Baadaye polisi waliwavamia na kuwatawanya.

“Tunaomba mumfikishie ujumbe Julio, hatumtaki, aondoke zake, anatuharibia timu yetu. Amuachie Kibadeni aendelee nayo,” alisikika mmoja wa mashabiki hao.
mwisho

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic