Benchi la ufundi la kikosi cha Simba,
limetamka kuwa tumu yao ipo kamili kabla ya kuwavaa Maafande wa Magereza,
Tanzania Prisons ya Mbeya kesho, lakini ukatoa tahadhari juu ya jambo moja.
Kocha Msaidizi wa Simba Jamhuri
Kihwelo ‘Julio, ameiambia Salehjembe kuwa
timu yao imefanya maandalizi ya kutosha katika kuelekea katika mchezo wa kesho,
utakaopigwa katika Uwanja wa Taifa jijini Dar, ambapo wataingia wakiwa na lengo
moja, kusaka pointi tatu muhimu.
Julio, amesema kila mchezaji wa timu
hiyo, inayoongoza ligi ikiwa na pointi 15, baada ya kushuka dimbani mara saba,
yupo katika hali nzuri, lakini wanahofia taarifa za wapinzani wao wa jadi Yanga,
kuwaharibia mipango yao hiyo, kufuatia kuwepo kwa taarifa za kupanga mikakati
ya kukihujumu kikosi cha Wekundu hao.
“Hatuna tatizo kila kitu kinakwenda
vizuri, tumefanya maandalizi ya kutosha, hatuna majeruhi yoyote katika kikosi
chetu, tunawaheshimu wapinzani wetu Prisons, tutaingia uwanjani kutaka pointi
tatu muhimu, ingawa tunajua kuwa soka ina matokeo ya aina tatu,” alisema Julio
na kuongeza:
“Mchezo wa soka una mambo mengi,
wakati mwingine fitina hazikosekani na hivi sasa, kuna taarifa nyingi kuwa wapo
wapinzani wetu wana nia ya kutaka kutuharibia mipango yetu, lakini Simba ipo
imara kupambana na kila changamoto.
acha uoga julio
ReplyDelete