Al Alhy imefanikiwa kutwaa ubingwa wa Afrika baada ya
kuichapa Orlando Pirates kwa mabao 2-0.
Timu hiyo kongwe ya Misri sasa imetwaa ubingwa kwa mara ya
nane.
Katika mechi ya awali, timu hizo zilitoka sare ya bao 1-1
jijini Johannesburg nchini Afrika Kusini. Kwa ushindi wa leo maana yake Al Ahly
imeshinda kwa jumla ya mabao 3-1.
Bao la kwanza la Ahly lilifungwa na mkongwe Mohammed Aboutrika kabla ya Ahmed Abdel Zaher hajamalizia kazi.
Hata hivyo Orlando Pirates ilijitahidi kupambana ili kuibwaga
timu hiyo kongwe kutoka Afrika Kaskazini lakini hakukuwa na mabadiliko.
0 COMMENTS:
Post a Comment