AFIF (KULIA) AKIWA NA ZAMOYONI MOGELLA WAKATI WAKIWA SIMBA PAMOJA |
Kocha wa zamani wa Simba, Hassan Afif
yuko nchini Hispania ambako ameamua kujiendeleza zaidi.
Akizungumza kutoka Hispania, Afif ambaye
sasa anafanya kazi zake nchini Qatar amesema tayari ameanza masomo.
“Nitakuwa huku kwa miezi sita, nimeamua
kujiendeleza zaidi kwa kuwa dunia inakwenda kwa kasi.
“Soka ya sasa kila siku mambo mapya na
tunachojaribu ni kupambana vilivyo na kujiendeleza pia,” alisema.
Afif alipata umaarufu mkubwa akiwa kocha
mchezaji wa Simba, mara nyingi alikaa kwenye benchi na kila alipoingia alitoa
pasi iliyozaa bao na hasa kwa mshambuliaji Zamoyoni Mogella.
Pamoja na kuwa mtoaji mzuri wa pasi
zilizozaa mabao, Afif pia alikuwa na uwezo mkubwa wa kufunga mabao muhimu.
0 COMMENTS:
Post a Comment