DILUNGA MAZOEZINI STARS |
Kiungo wa Ruvu Shooting, Hassan Dilunga
ameikana Yanga na kushangazwa na taarifa zilizotolewa na mtandao wa timu hiyo
na kusambazwa.
Mtandao wa Yanga pamoja na wall yake ya
Facebook ilieleza tayari uongozi umemtia Dilunga mkononi.
Lakini alipoulizwa leo katika mazoezi ya
Stars akasema: “Nashangazwa na taarifa hizo, hakika bado ni mchezaji wa Ruvu
Shooting.
“Unakumbuka mwaka jana, walisema
nimesaini Simba lakini mwisho nilicheza timu gani? Uliona mwenyewe. Mimi sijasaini
Yanga.”
0 COMMENTS:
Post a Comment