Pamoja
na kuondolewa kazini, aliyekuwa Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Osiah ataendelea
kulipwa mshahara.
Kwa
mujibu wa Rais wa TFF, Jamal Malinzi, katibu huyo wa zamani ataendelea kulipwa
mshahara kwa muda huo ambao ndiyo mkataba wake utamalizika.
“Ataendelea
kupata haki kama kawaida na baada ya hapo tutakuwa tumemalizana,” alisema.
Kuhusiana
na Boniface Wambura ambaye amepewa nafasi ya kukaimu nafasi hiyo Osiah, Malinzi
amepomba apewe ushirikiano.
“Kamati ya Utendaji inaziomba klabu, vyama vya wilaya, vyama vya
mikoa, vyama shiriki na wadau wote kumpa ushirikiano Boniface Wambura katika
utekelezaji wa majukumu yake,” alisema Malinzi leo asubuhi.
0 COMMENTS:
Post a Comment