Kocha Mkuu wa Yanga, Ernie Brandts
amesema kikosi chake kingeweza kuichapa JKT hata mabao sita kama kingekuwa
makini.
Hata hivyo akasema amefurahishwa na
ushindi wa mabao 4-0 katika mechi hiyo ya Ligi Kuu Bara kwenye Uwanja wa Taifa,
leo.
“Ilikuwa mechi ambayo timu yangu ilikuwa
imebadilika kiuchezaji kama utalinganisha na mechi zilizopita, tulicheza
vizuri.
“Lakini tatizo kubwa tulishindwa kutumia
nafasi tulizozipata, ndiyo kitu muhimu ambacho tunapaswa kukifanyia kazi ili
kuendelea kujikita kileleni.
“JKT walikuwa wazuri, hilo hatudharau
lakini kikosi change kilicheza vizuri zaidi katika mechi ya leo,” alisema
Brandts.
Mabao manne ya Yanga katika mechi ya leo
yalifungwa na Mrisho Ngassa (mawili), Oscar Joshua na Jerry Tegete.
0 COMMENTS:
Post a Comment