Zanzibar Heroes imeanza vizuri michuano ya Kombe la
Chalenji baada ya kuichapa Sudan Kusini kwa mabao 2-1.
Zanzibar Heroes imeshinda mechi yake hiyo ya ufunguzi
dhidi ya Sudan Kusini kwenye Uwanja wa Nyayo jijini Nairobi, leo.
Mechi hiyo ilikuwa nzuri, Zanzibar wakitawala zaidi na
kama wangekuwa makini wangeweza kushinda mabao mengi zaidi.
Wao ndiyo walitangulia kufunga mabao yote mawili kabla ya
Sudan Kusini kupata la kufutia machozi.
0 COMMENTS:
Post a Comment