KOCHA MCHEZAJI WA GLOBAL, SALEH ALLY AKIMTOKA BEKI WA BAGAMOYO VETERANI WAKATI TIMU HIYO ILIPOIVAA TASWA FC, MWAKA JANA. |
Na Shafii Hashim
Baada ya wikiendi iliyopita timu ya
Global Publishers FC kuibuka na ushindi wa kibabe wa bao 1-0 dhidi ya Chuo cha
Dar es Salaam City (Dacico), kesho Jumamosi timu hiyo inatarajiwa kuelekeza
nguvu zake kwenye mechi yao kabambe dhidi ya Bagamoyo Veterani.
Mechi hiyo itakayopigwa Bagamoyo,
Pwani, ni moja kati ya ziara nyingi za mikoani za kimichezo za timu hiyo
zinazotarajiwa kufanyika hivi karibuni ili kukiweka sawa kikosi kwa ajili ya
michuano mingi ya kuufunga mwaka 2013 na kuukaribisha 2014.
Nahodha wa timu hiyo yenye maskani
yake maeneo ya Mwenge jijini Dar, Phillip Nkini ameliambia gazeti hili kuwa,
mara baada ya mechi ya Bagamoyo, ziara yao hiyo itaendelea kwenye mikoa ya
Tanga, Morogoro na visiwani Zanzibar.
Alisema wakiwa huko, wachezaji wa
Global ambao pia ni waandishi wa Gazeti la Championi, watapata fursa ya kuzungumza
na wasomaji wao kujua wanahitaji nini zaidi kwenye magazeti ya Championi ili
wazidi kulifurahia zaidi gazeti hilo bora la michezo Tanzania.
“Baada ya mechi ya Bagamoyo,
tutaelekea Tanga, Morogoro na Zanzibar kwa ajili ya kwenda kukipiga huko na
kuzungumza na wasomaji wetu,” alisema Nkini.
0 COMMENTS:
Post a Comment