November 29, 2013





Adhabu ya Simba kutakiwa kulipa Sh milioni 25 kutokana na mashabiki wake kung’oa viti kwenye Uwanja wa Taifa, huenda ikaongezeka kwa kuwa mpaka sasa haijalipwa.


Moja ya adhabu ambazo zimezungumzwa ni kuwa, kuna uwezekano wa kucheza mechi sita bila mashabiki.

Mkurugenzi wa Mashindano wa Shirikisho la Soka la Tanzania (TFF), Saad Kawemba, alisema suala la Simba linatarajiwa kujadiliwa na kamati ya nidhamu ya TFF ambayo bado haijaundwa.

Lakini amesisitiza kuwa, kabla ya uamuzi wowote wa adhabu ya ziada, pande zote tatu; serikali, Simba na TFF, zitakutana kwa ajili ya mazungumzo.

“Kamati ya Nidhamu ya TFF itakapoundwa ndipo suala lao litakapojadiliwa zaidi ili kujua kama adhabu itaongezeka au itapunguzwa, kwani hadi sasa kamati hiyo haijaundwa.

“Kwani yanaweza yakatolewa maamuzi ya kucheza mechi sita bila mashabiki iwapo tutaona adhabu iliyotolewa awali haitoshi kulingana na kosa lenyewe,” alisema Kawemba.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic