IVO AKIWA MAZOEZINI KWENYE UWANJA WA CITY JIJINI NAIROBI, LEO ASUBUHI |
Na Saleh Ally, Nairobi
Kipa wa Gor Mahia ya Kenya, Ivo Mapunda
amesema amekuwa maarufu sana jijini hapa hata kuliko ilivyokuwa jijini Dar.
Akizungumza jijini hapa, Ivo amesema
amekuwa akipata sapoti kubwa kutoka kwa mashabiki wa Gor Mahia.
“Ninaishi vizuri sana hapa, ninaelewana
na watu wengi na kweli nimekuwa maarufu mno.
Watu wananiamini na tunaheshimiana sana,
ninaishi maisha mazuri na nina furaha sana,” alisema Ivo katika mahojiano
maalum.
Katika mitaa ya Nairobi, Ivo amekuwa
maarufu sana kutokana na uwezo mkubwa aliouonyesha.
Msimu huu ameisaidia Gor Mahia kubeba
ubingwa wa Ligi Kuu Kenya ikiwa ni zaidi ya miaka 10 tokea walipoubeba kwa mara
ya mwisho.
0 COMMENTS:
Post a Comment