Kamati ya utendaji ya Simba ilikutana
jana jioni na kujadili masuala kadhaa likiwemo la kubaki au kuondoka kwa kocha
msaidizi wake, Jamhuri Kihwelo ‘Julio’.
Taarifa zinaeleza kwamba huenda Julio
akafutwa kazi kutokana na kuonekana analalamikiwa sana na wachezaji.
Taarifa zinaeleza huenda Julio akaondoka
Simba mara tu baada ya mechi ya mwisho ya Simba katika mzunguko wa kwanza.
“Sidhani kama Julio atarudi katika
mzunguko wa pili, lakini ni suala ambalo linaendelea kujadiliwa,” kilieleza
chanzo.
Julio ni msaidizi wa Abdallah Kibadeni
na taarifa zinaeleza pia alijadiliwa katika kikao hicho lakini bado hakukuwa na
jibu.
0 COMMENTS:
Post a Comment