Taarifa za kipa nyota, Juma Kaseja kutua
Yanga zimewachanganya watu wengi.
Ingawa zimekuwa hazina uhakika, lakini
Salehjembe imepata taarifa za uhakika kwamba mchana huu ndiyo amemalizana na
Yanga.
Lakini bado watu wamekuwa wakihaha
kutaka kujua kuhusiana na suala hilo.
Mmoja wa viongozi wa Yanga alisema; “Sitaki
kulizungumzia kwa sasa, kama kuna walioandika sawa, lakini kumalizana kwetu na
Juma ni leo (Alhamisi).
“Tulimpa mkataba, anao yeye, hivyo
tutakutana na kumalizana leo na tumegawanya makundi mawili, moja litakuwa
uwanjani katika mechi dhidi ya Oljoro na lingine katika ishu hiyo ya Kaseja.”
mpira kaz acha akafanye kaz
ReplyDelete