November 7, 2013



Mabingwa wa soka Tanzania Bara, Yanga wamepaa kileleni mwa ligi kuu ikiwa ndiyo mwisho wa mzunguko wa kwanza.


Yanga imeshika usukani kwa kufikisha pointi 28 kutokana na kipigo walichoipa JKT Oljoro cha mabao 3-0 leo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar.

Kabla ya hapo Azam FC ilikuwa inaongoza ligi hiyo ikiwa na pointi 26, sawa na Mbeya City iliyokuwa katika nafasi ya pili.
Lakini timu hizo mbili zimetoka sare ya bao 3-3 leo kwenye Uwanja wa Chamazi Complex na kila moja zimebaki na pointi 27.

Maana yake, Azam FC inabaki katika nafasi ya pili na Mbeya City tatu ikiwa ni tatu na zinatofautiana mabao ya kufunga na kufungwa ‘GD’.

SImba inabaki katika nafasi ya nne ikiwa na pointi 24 ilizofikisha baada ya ushindi wa jana wa mabao 4-2 dhidi ya Ashanti United.

Katika mechi ya leo, mabao ya Yanga yalifungwa na Simon Msuva katika dakika ya 23, Mrisho Ngassa akaongeza bao katika dakika ya 30 na Jerry Tegete katika dakika ya 54.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic