TUNAJARIBU TU |
Bingwa wa dunia, Francis Cheka leo
amenitembelea ofisini kwangu.
Pamoja na majukumu mengi ya gazeti la
Championi nilimpa muda na tukazungumza na kujadiliana mambo kadhaa.
Urafiki na undugu wetu umeanza miaka
kadhaa akiwa bondia wa ngumi za ridhaa.
Kanieleza mambo kadhaa, lakini kauli
yake hii: “tusimlaumu Matumla kulalamika leo, wala tusione aliyatumia maisha
vibaya.
“Mabondia hatulipwi vizuri na fedha
nyingi tunamalizia katika maandalizi.
TUKIWA NA JOHN JOSEPH WA CHAMPIONI |
AKIWA NA WILBERT MOLANDI WA CHAMPIONI |
“Angalia mimi leo ni bingwa wa dunia
lakini hakuna faida kubwa kwenye malipo. Hili suala linaniumiza sana kichwa kwa
kuwa sitakuwa juu siku zote.
“Itafikia siku nitakuwa kama Matumla,
hivyo vyama na mashirikisho ya ngumi yatupiganie.”
Hakika niliona ana hoja ya msingi na
ninaona wahusika wanapaswa kuifanyia kazi.
0 COMMENTS:
Post a Comment