Kwa mara ya kwanza, kikosi cha U 20 cha
Yanga kimefanikiwa kutinga fainali ya michuano ya Uhai Cup.
Yanga imefanikiwa kuingia fainali hivi
punde baada ya kuichapa Mtibwa Sugar kwa mabao 3-1.
Sasa itacheza na Costal Union iliyoivua ubingwa Azam FC. Mechi hiyo ya fainali itapigwa keshokutwa Jumapili.
Katika mechi hiyo iliyochezwa Chamazi,
Yanga inayofundishwa na Salvatory Edward, ilionyesha kuutawala mchezo kuanzia
mwanzo.
Yanga imeimaliza Mtibwa Sugar katika
mechi hiyo ya nusu fainali baada ya timu hiyo ya Manungu kuing’oa Simba katika
fainali.
PICHA NA LENZI YA MICHEZO
0 COMMENTS:
Post a Comment