Na Saleh
Ally
Wakongwe wa
soka nchini, Yanga na Simba, ndiyo timu gumzo kuliko nyingine zote nchini na
zinaingia katika kila linalozungumziwa kwenye mchezo huo nchini.
Yanga na
Simba ndizo zinachangia kwa kiasi kikubwa mchezo wa soka nchini, lakini ndizo
zinazohusika katika lawama ya kuporomoka kwa mchezo huo.
Kama
utasikia suala la kuharibika kwa mambo katika mchezo wa soka, basi Simba na
Yanga hawawezi kukosekana na yote hayo yanatokana na mambo mawili makubwa.
Kwanza ni
wivu wa kawaida ya timu hizo kutaka kuwa juu siku zote hata kama hazijitumi,
ndiyo maana Yanga au Simba itaona bora ubingwa uchukuliwe na mmoja wao kuliko
timu nyingine.
Pili ni
mapenzi binafsi, maana hata viongozi wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) na
wale wa serikali, wapo katika makundi mawili kama mashabiki wa kawaida.
Simba na
Yanga haziwezi kukwepa hilo, lakini ukirudi katika suala la maendeleo, si
sahihi kuziacha na lawama ziwe kama mafuriko kwao, badala yake wakati mwingine
zinastahili pongezi.
Maendeleo:
Maendeleo
ya karibu asilimia 90 yamepatikana kupitia timu hizo, utaona zikiwa uwanjani
zinasukuma ‘gozi la ng’ombe’ lakini ukweli zenyewe ndiyo wafalme wa mengi
mazuri yanayopatikana.
Mfano,
mapato kila zinapocheza yanapatikana kwa wingi zaidi kuliko inapocheza timu
nyingine yoyote.
Yanga na
Simba, kila moja imecheza mechi 13 za mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu Bara,
hakuna hata timu moja imefikia nusu ya kila kilichofanyika kwao kwa maana ya
faida.
Kama
utazungumzia mapato, idadi ya watu zilizoingiza uwanjani, utaona hakuna hata
timu iliyofanikiwa kunusa nusu ya zilivyofanikiwa, hii ni sehemu ya kuonyesha
ubora wao, hata kama kuna sehemu zinaharibu.
Mapato:
Yanga ndiyo
imeongoza kwa mashabiki na kiwango cha mapato, Sh milioni 334.2 katika mechi
zote 13, Simba Sh milioni 304 na Mbeya City ikashika nafasi ya tatu na Sh
milioni 83.8.
Mapato hayo
ni baada ya makato yote, lakini kabla ya makato makubwa, Yanga na Simba, kila
moja imeingiza zaidi ya Sh bilioni moja katika mechi hizo 13.
Angalia
Mbeya City iliyoshika nafasi ya tatu kwa mapato, imeshindwa kuingiza hata nusu
ya fedha ambazo wameingiza Yanga na Simba (kila moja). Huu ni mfano mzuri
kwamba timu hizo zinachukua mapenzi ya wapenda soka wengi.
Uwanja wa
Taifa jijini Dar es Salaam ndiyo umeongoza kwa kuingiza mapato makubwa zaidi,
Sh bilioni 1.8 si mchezo na hii ni kwa kuwa unatumiwa na timu hizo kongwe.
Uwanja wa
Sokoine, Mbeya unaotumiwa na timu za Prisons na Mbeya City umeibuka na kushika
nafasi ya pili kwa kuingiza Sh milioni 260.5. Hii ni robo tu ya mapato ya Taifa.
Mbeya
wamejitahidi na hayo ni mabadiliko ya kuwepo Mbeya City, lakini hakuna ubishi
tena kuwa Yanga na Simba ndizo zinazoendesha mapato ya soka nchini.
Mashabiki:
Katika
mechi ambazo Yanga au Simba wamekuwa wenyeji au wanacheza, ndizo mashabiki walizojitokeza
kwa wingi kuliko timu nyingine na huu ni uthibitisho wa mvuto wao kwa
mashabiki.
Yanga
imeonyesha kuwa na mvuto zaidi kwa kufuatwa na mashabiki 107,890, Simba
inafuatia kwa mashabiki 97,364, Mbeya City
43,439 na Azam FC 30,236.
Hapa bado
heshima kwa timu hizo kwamba ndizo zenye mvuto zaidi kwa mashabiki nchini, pia
takwimu hizo zinamaliza ubishi kuwa Yanga ndiyo yenye mvuto zaidi kwa maana ya
mashabiki.
Yanga na Simba ndiyo chachu ya mafanikio ya
soka nchini, huenda zinageuka kuwa sumu kutokana na mfumo wa wanaoziendesha na
hasa viongozi. Lakini zikitumika vizuri, basi zinaweza kuwa changamoto ya
maendeleo maradufu.
Angalia namna zilivyotesa kwenye mapato na
wingi wa mashabiki huku kukiwa hakuna timu iliyosogea na kunusa hata nusu yao.
MAPATO KWA
TIMU
Yanga
imekusanya Sh 334.2m
Simba
imekusanya Sh 304m
Mbeya City
imekusanya Sh 83.8m
Azam FC Sh 67.1m
Coastal
Union Sh 65.7m
Mtibwa
Sugar Sh 49.9m
Ruvu
Shooting Sh 46.1m
Tanzania
Prisons Sh 38.1m
JKT Ruvu Sh
36.1m
Ashanti
United Sh 35.7m
Rhino
Rangers 31.1m
Mgambo JKT Sh
25.8m
Oljoro JKT Sh
20.8m
Kagera
Sugar Sh 18.5m
IDADI YA
MASHABIKI:
Yanga-107,890
Simba-
97,364
Mbeya City-
43,439
Azam FC-30,236
Coastal-27,880
Mtibwa-Sugar
20,794
Rhino
Rangers -20,263
Prisons-19,923
Ruvu
Shooting -19,000
JKT Ruvu-16,095
Ashanti-16,093
Mgambo-11,726
JKT Oljoro-10,430
FEDHA
AMBAZO VIWANJA ZIMEINGIZA…
Uwanja wa
Taifa (Dar) Sh bilioni 1.8
Sokoine (Mbeya)
Sh milioni 260.5
Mkwakwani (Tanga)
Sh milioni 105.3
Ali Hassan
Mwinyi (Tabora) Sh milioni 100.2
Sheikh Amri
Abeid (Arusha) 57.4
Azam
Complex (Dar) Sh milioni 32.1
Kaitaba (Bukoba)
Sh milioni 26.1
Manungu (Turiani)
Sh milioni 9.4
Mabatini (Mlandizi)
Sh milioni 3.9
0 COMMENTS:
Post a Comment