Kocha Patrick
Liewig aliyewahi kuinoa Simba, amesema timu hiyo itaendelea kufanya vibaya.
Liewig raia
wa Ufaransa, amesema Simba itaendelea kufanya vibaya kwa kuwa kikosi chake bado
hakijawa imara lakini ajabu hata ushirikiano haupo.
“Nimeona
Simba ikicheza, angalau hata msimu uliopita ilikuwa ina kiwango kizuri.
“Nilitegemea
msimu huu kuwe na mabadiliko makubwa, lakini mambo ni tofauti. Nimekuwa nikisikia
wanazozana na wachezaji wengine kushushwa daraja wakati wana uzoefu na
wanahitajika.
“Huenda
sijaelewa kinachoendelea, lakini itakuwa vizuri sana kama watadumisha zaidi
ushirikiano na kutafuta njia ya kuyatatua matatizo ya ndani bila kuongeza
misuguano.
“Ugomvi
husababisha hofu na mwisho unajenga uoga, hivyo wanatakiwa kuwa makini,”
alisema Liewig ambaye alirejea nchini kwa ajili ya kudai fedha zake.
0 COMMENTS:
Post a Comment