Kocha Mkuu wa
Yanga, Ernie Brandts amesema kuwa kikosi chake kiwe bingwa wa Ligi Kuu Tanzania
Bara, basi wanahitaji kushinda mechi zote walizobakisha.
Brandts raia
wa Uholanzi amesema hayo ndiyo malengo aliyoyaweka yeye na benchi lake la
ufundi katika mechi hizo.
“Ili
tujiwekee mazingira mazuri ya ubingwa, basi tunahitaji tushinde kila mechi
tutakayocheza. Hayo ndiyo malengo tuliyojiwekea kwenye msimu huu, ninaamini
hilo litafanikiwa kutokana na ubora wa kikosi changu na ushirikiano ninaoupata
kwenye benchi langu la ufundi,” alisema Brandts.
Aidha, Brandts
amesema kuwa alimpa nafasi ya kucheza kwa dakika 10 mshambuliaji Lusajo
Reliants katika mechi dhidi ya Mgambo kwenye Uwanja wa Taifa, Jumanne wiki hii
ili kuona kiwango chake, na kusisitiza kuwa ataendelea kumpa nafasi kidogo ili awe
katika hali ya mchezo.
Kweli
alifanya hivyo tena katika mechi ya jana wakati Yanga ilipoivaa JKT Ruvu na
kushinda mabao 4-0 dhidi ya JKT Ruvu.
0 COMMENTS:
Post a Comment