Kipa mpya wa Yanga, Juma Kaseja
alichelewa kusaini kwa takribani siku nne kutokana na suala la matangazo.
Kipingele kinachohusiana na matangazo
ndani mkataba huo wa Yanga kilitakiwa kuondolewa.
Baada ya kukutana na kukubaliana,
Kaseja aliomba mkataba wake kwanza ausome.
Lakini aliporudishwa, kipengele hicho
bado kilikuwa hewani.
“Aliporudishiwa kile kipengele bado
haikutolewa, ndiyo ma ana Juma alikuwa anajaribu kukwepakwepa.
“Lakini baadaye aliwaambia Yanga moja
kwa moja kwamba anahitaji marekebisho ndiyo asaini na wao wakafanya hivyo
walipokutana, kweli akasaidia.
“Sasa Juma ni mchezaji halali wa Yanga,”
kilieleza chanzo.
Hata hivyo haikuwelezwa kipengele hicho
kama kilikuwa kinamzuia Kaseja kufanya matangazo au la.
Kaseja ana mkataba na kampuni ya
viwaywaji baridi ya Pepsi Cola.
0 COMMENTS:
Post a Comment