Denis Oliech amekuwa mchezaji wa kwanza
wa kutoka nje ya Kenya ambaye ametua jijini hapa kwa ajili ya kujiunga na timu
ya taifa.
Timu ya taifa ya Kenya, Harambee Stars Novemba
14 inatarajia kukipiga na Oman katika mechi ya kirafiki itakayochezwa jijini
Muscat, Oman.
kocha Mkuu wa Harambee Stars, Adel Amrouche amesema amazungumza na mshambuliaji huyo na tayari yuko jijini hapa.
Oliech ni kati ya wachezaji walioitwa
na Kocha Adel Amrouche lakini haikuwa kawaida yake kuwahi.
Mshambuliaji huyo anayekipiga nchini
Ufaransa, ametua jijini hapa na tayari amekuwa gumzo kutokana na kurejea kwake.
0 COMMENTS:
Post a Comment