Mwanamuziki maarufu wa kike, Shakira na
kipenzi chake, beki wa Barcelona, Gerard Pique wamezidi kuonyesha kuwa penzi
lao liko hai baada ya kujitokeza katika mechi ya mpira wa kikapu.
Mechi hiyo, timu ya Barcelona ilikuwa
inacheza dhidi ya Fenerbahce Ulker Istanbul kwenye Uwanja wa Palau Blaugrana jijini Barcelona.
Wawili hao walionekana kuwa karibu na
kujadili mambo kadhaa huku mkono wa Shakira ukiwa katika paja la mpenzi wake
huo muda wote.
Hivi karibuni kulikuwa na taarifa
kwamba wako kwenye mfarakano ndiyo maana siku nyingi hawajaonekana pamoja.
Kutokea tena wakiwa wenye furaha,
inaonyesha wazi ni kama jibu la waliokuwa wakieleza kwamba wako katika
mtafaruku.
0 COMMENTS:
Post a Comment