November 30, 2013

AKIKABIDHIWA JEZI NA MWENYEKITI WA AZAM FC, SAID MOHAMMED

Kocha mpya wa Azam FC Joseph Omog hatimaye leo ametua rasmi jijini Dar tayari kwa kuanza kazi ya kukinoa kikosi hicho.
Omog raia wa Cameroon ametua leo saa 3:00 asubuhi na Ndege ya Shirika la Kenya ambapo mara baada ya kuwasili alipelekwa moja kwa moja katika ofisi kuu za timu hiyo zilizopo Mzizima na kusaini mkataba wa miaka miwili.


Mara baada ya kusaini mkataba huo Omog anayechukua nafasi ya Muingereza Stewart Hall alitambulishwa rasmi kwa waandishi wa habari na mwenyekiti wa timu hiyo Said Mohamed ambaye alimtaja kocha huyo kuwa ni kati ya makocha bora sita wanaopatikana Bara la Afrika.
AKIKARIBISHWA BAADA YA KUWASILI NA MENEJA WA AZAM FC, PATRICK KAHEMELE

Mohamed maarufu kama Mzee Said amesema Azam inafuraha kubwa kumpata Omog ambaye uongozi wa timu hiyo umeona ndiye anayestahili kuchukua nafasi ya Stewart aliyesitisha mkataba mwezi uliopita.

Omog kwa upande wake kocha wa zamani wa kikosi cha AC Leopards ya Congo Brazaville alionyesha kushangazwa na mapokezi aliyoyapata ambapo amesema mara baad ya kusaini mkataba huo sasa kazi yake kubwa ni kuhakikisha timu hiyo inaoata mafanikio ndani ya uwanja.


Kivutio kikubwa katika ujio wa kocha huyo ni kuja na mwanaye Henry Omog ambaye ni beki wa zamani wa  Canon de Yaunde huku akiwa ndiye meneja wa baba yake huyo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic