WAZIRI MAKAMBA AKIZUNGUMZA |
Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Januari
Makamba amewasifu kampuni ya Azam Group na kusema anaamini Azam Media itafanya
vizuri sana.
Akizungumza katika uzinduzi wa Azam TV jana kwenye hoteli ya
Hayat jijni Dar, Januari ambaye ni mbunge wa Bumbuli alisema anaamini runinga
hiyo itapata mafanikio makubwa.
WAKATI WA UZINDUZI |
“Kila wanachokugusa Azam kinakubali na kupata mafanikio,
ninaamini hata Azam TV itafanikiwa sana,” alisema.
“Tunawaamini Azam kwa kila wanachogusa, lakini kitu muhimu ni
content, hivyo wajitahidi kuwa na vitu vinavyowagusa watazamaji wao na hasa
Watanzania.
MMOJA WA WAKURUGENZI WA AZAM TV, YUSUF BAKHRESA (MWENYE SUTI) AKIWA KWENYE UZINDUZI HUO. |
“Watu wamekuwa wakilaumu kwa kila kitu, lakini bado vitu
vinaanzishwa kama unavyoona Azam TV inaanzishwa. Vizuri tukajivunia, kama
walivyosema wenyewe hii ni runinga ya kimataifa inayotokea Tanzania,” alisema.
Kabla Azam TV ilizindua king’amuzi chake chenye chaneli
takribani 50 ambacho kitakuwa kinalipiwa Sh 12,500 tu kwa mwezi.
0 COMMENTS:
Post a Comment