BERKO MARA TU BAADA YA KUWASILI UWANJA WA NDEGE WA KIMATAIFA WA JULIUS NYERERE JIJINI DAR |
Aliyekuwa kipa wa Yanga Mghana Yaw
Berko ametua leo jijini Dar tayari ya kuanza maisha mpya na Simba SC.
Berko ametua jijini leo asubuhi
na ndege ya Shirika la Kenya akitokea kwao Ghana na kulakiwa na kiongozi wa
ufundi wa Simba, Danny Manembe.
Mara baad ya kutua Berko alipata
nafasi ya kuzungumza na Salehjembe akisema anaijua Simba vizuri huku pia
akimjua kipa wao namba moja Abel Dhaira ambapo atahakikisha anapambana katika
mazoezi ili kujihakikishia nafasi katika timu hiyo.
“Naijua Simba, mimi sio mgeni hapa,
namjua pia kipa wao yule wa Uganda lakini namtanguliza Mungu, lakini pia
nitajituma mazoezini ili kuweza kujipatia nafasi.
0 COMMENTS:
Post a Comment