Tottenham
Hotspur imenyoosha darubini zake kuanza kumvizia kocha Luis Enrique aliyewahi
kukipiga Barcelona.
Dalili
kwamba kocha Andre Villas-Boas amekalia kuti kavu baada ya timu yake kukutana
na kipigo kikali cha Man City.
Mjadala
ni kwamba timu hiyo ilifanya usajili wa pauni milioni107 lakini imekuwa
haionyeshi mafanikio yoyote.
Enrique
amerudi Hispania kuisaidia Celta Vigo na aliwahi kufanya kazi na mkurugenzi wa
soka wa Spurs, Franco Baldini wakati wakiwa Roma.
Pia
aliwahi kuifundisha kwa mafanikio makubwa Barcelona B kabla ya kuiacha timu
hiyo na kwenda kufanya kazi Roma.
kocha mwingine anayewaniwa ni Michael Laudrap anayeinoa Swansea na
imeelezwa alikuwa njiani kuiacha timu hiyo.
0 COMMENTS:
Post a Comment