Mabingwa Yanga wameendelea kuongeza kasi
ya kusaka pointi katika Ligi Kuu Bara baada ya kuibutua Ruvu Shooting kwa mabao
4-0.
Mabao ya Yanga yamefungwa na Mrisho
Ngassa aliyepiga mawili, Oscar Joshua na Jerry Tegete aliyeingia kipindi cha
pili.
Muda mwingi Yanga walitawala mchezo huo
lakini walipoteza nafasi nyingi za kufunga mabao ambazo zingeweza kuwapa mabao
mengi zaidi.
Muda mwingi JKT walionekana kupoteana na
kutoa nafasi kwa Yanga kucheza wanavyotaka lakini tatizo lilikuwa ni kuzitumia
nafasi hizo.
0 COMMENTS:
Post a Comment