Nimeikuta hii picha kwenye wall ya
facebook ya Mwani Nyangasa, dada na mshikaji. Nimefurahi sana kwa kuwa sina
picha bora kama hii nikiwa kazini, badala yake nimekuwa nikiwapiga wengine tu.
Nimefurahi sana, hehe. Kumbe namna hii
ndiyo hufanya kazi, nasikia raha kwa kuwa ndiye kiongozi pekee wa gazeti ambaye
amekuwa akipiga picha, bosi wa wahariri anayeweza kukubali kwenda mtaani
kutafuta stori na kupiga picha.
Wakati mwingine wahariri ambao mimi ni
bosi wao, hunipa kazi ya kupiga picha, ninaenda na kurudi na kazi safi kabisa.
Ninaamini hata wengine wanaochipukia au
wale wakongwe wanaweza kujifunza katika hili. Namshukuru Mwenyezi Mungu kwa
uwezo mzuri alionipa, kila kukicha nang’amua mengi na ninaendelea kujifunza. Daima
siwezi kuvimba kichwa kwa kuwa kama ni hivyo, ningekuwa nimepotea siku nyingi.
Kama ningekuwa mjinga ningevimba kichwa
kwa kuwa nimefanya mengi sana katika uandishi wa michezo na wengi hawajafikia.
Mahojiano
na wachezaji wengi wakubwa kama Kolo Toure, Yaya Toure, Didier Drogba, Steven
Pierneer, Samuel Eto’o, Salmon Kalou, Emmanuel Ebou na wengine wengi ambao hata nimesahau.
Makocha kibao kama Pitso Mosimane, Gareth Southget, Sabri
Lamouch, Marcelo Lippi, Dunga na wengine wengi tu lakini hadi leo niko kawaida
na ninaendelea kupiga kazi kama zamani.
Nashukuru kwa kujitambua, nakushukuru
Mwani kwa picha nzuri. Ahsante mnaoniunga mkono kwa kunisapoti, siku zote napokea changamoto na ushauri.
AHSANTE SANA MUNGU KWA YOTE HAYA.
Aluta continua.
0 COMMENTS:
Post a Comment