December 13, 2013





Kocha Mkuu wa Simba, Zdravok Logarusic ‘Loga’ amesema mpaka kufikia sasa wakati timu yake ikiendelea kujifua, mchezaji anayemuona kuwa na uhakika wa namba kwenye safu ya ushambuliaji ni Uhuru Selemani.


Uhuru ambaye amerejea klabuni hapo baada ya kuichezea Coastal Union kwa mkopo, amekuwa akionyesha kiwango kizuri na kujituma katika mazoezi.

“Uhuru ni mchezaji mzuri uwanjani, ndiye naona ana uhakika wa namba kwenye ushambuliaji, labda sijui hapo baadaye kama atakuja kubadilika, lakini mpaka sasa ndiye anaona ananifaa mbele,” alisema Loga.

Uhuru alipelekwa Azam FC kwa mkopo kisha Coastal lakini kote alikuwa na wakati mgumu wa kupata namba kwenye kikosi cha kwanza.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic