Ashanti United ipo
kwenye mikakati ya kuiwania saini ya kiungo wa zamani wa Simba na Yanga,
Mohammed Banka kwa ajili ya kuiongezea nguvu timu hiyo kwenye mzunguko wa pili
wa Ligi Kuu Bara.
Imeelezwa kuwa, Banka amemaliza mkataba
wake na Bandari FC ya Kenya alikokuwa anacheza, hivyo yupo nchini kama mchezaji
huru huku timu nyingi, ukiacha Ashanti, nazo pia zikiulizia huduma yake.
Chanzo makini kutoka ndani ya Ashanti
kilisema timu hiyo inazungumza na mchezaji huyo ili iweze kuona kama itaweza
kumpata.
“Kuna wachezaji wanawataka lakini kwenye
orodha yao lipo pia jina la Banka na wanamtaka kutokana na uzoefu wake na
mchango wake kwenye soka, kwa hiyo kwa sasa wanajaribu kufanya naye mazungumzo
waone kama wanaweza kumnasa kwa sababu kuna timu nyingine pia zinamnyemelea,”
kilisema chanzo hicho.
Katibu Mkuu wa Villa, Mbarouk Kasanda,
amesema wameshafanya mazungumzo na kiungo huyo na kila kitu kinakwenda sawa, hivyo
wana asilimia 80 za kumnasa.
“Kilichobaki ni saini yake tu lakini
kila kitu kimekwenda kama kilivyopangwa, tumeshazungumza naye na yeye pia
ameafiki, kwa hiyo uhakika wa kuwa naye kwenye mzunguko wa pili ni asilimia 80,”
alisema Mbarouk.
0 COMMENTS:
Post a Comment