Kipa Yaw Berko raia wa Ghana anaonekana
kuanza kuyazoea mazingira ya ofisi yake mpya.
Leo asubuhi amefanya mazoezi akiwa na Simba kwa mara ya pili
lakini zaidi alionekana kuwa karibu na kiungo Henry Joseph.
Henry na Berko mara kadhaa walikuwa
wakibadilishana mawazo kila walipopata nafasi.
Hata kilipotokea kitu hakikumvutia,
Berko aliyewahi kuwa kipa wa Yanga alikuwa akimuita Henry na kuzungumza naye.
Kipa huyo, jana amesaini mkataba wa nusu
msimu kuichezea Simba na baada ya hapo ataondoka nchini.







0 COMMENTS:
Post a Comment