| NJOVU (KULIA) AKIWA NA MANJI, LEO. |
YANGA
imemtangaza Beno Njovu katibu mkuu wa klabu hiyo kongwe.
Kwa sasa
nafasi hiyo anaikaimu Lawrance Mwalusako, beki wa zamani wa Yanga.
Kabla ilikuwa
inashikiliwa na Selestine Mwesigwa ambaye aliondolewa na Mwenyekiti wa Klabu
hiyo, Yusuph Manji kwa kutoridhika na utendaji kazi wake klabuni hapo.
Njovu
ametangazwa leo na Maji kwenye makao makuu ya klabu hiyo. Kawaida nafasi hiyo
ni ya kuajiriwa.
Manji alisema
uamuzi wa kumteua Njovu katika nafasi hiyo umefikiwa na kamati ya utendaji.
Aidha, alisema
kuwa Njovu ameanza kazi rasmi jana mara baada ya kutangazwa kwenye makao makuu
ya klabu hiyo yaliyopo Kariakoo jijini Dar na kwamba atakabidhiwa Ofisi na
Mwalusako Januari 19, mwakani siku ya Mkutano Mkuu wa klabu hiyo.







0 COMMENTS:
Post a Comment