December 10, 2013




Mwenyekiti wa Klabu ya Yanga, Yusuph Manji ametangaza rasmi kutowania tena nafasi ya uenyekiti kwenye uchaguzi mkuu wa klabu hiyo utakaotangazwa baadae mwakani.


Manji ametoa ametoa tamko kuhusiana na suala hilo alipozungumza na waandishi kwenye makao makuu ya klabu hiyo yaliyopo Jangwani, Kariakoo jijini Dar es Salaam.
Manji amesema ameamua kuwapisha  wengine wenye uwezo wa kuiongoza timu hiyo nao kuchukua jahazi.

“Sitagombea tena uenyekiti kwenye uchaguzi ujao, nimetangaza ili kuwapisha watu wengine ambao wana uwezo waingie na kuendeleza kutoka nilipoishia,” alisema.

Manji ataendelea kuwa kiongozi wa Yanga kwa miezi ijayo saba hadi hapo utakapoitishwa uchaguzi huo, hapo mwakani.
Manji amesisitiza, baada ya muda huo kwisha naye kutogombea, basi angependa kuendelea kubaki kama mwanachama na shabiki wa kawaida.

Taarifa za uamuzi huo wa Manji huenda zikawashtua wanachama wa Yanga ambao walionyesha kufurahishwa na mabadiliko aliyoyafanya.
Manji aliamua kugombea siku chache baada ya Yanga kupoteza mechi yao ya Ligi Kuu Bara dhidi ya Simba kwa kufungwa mabao 5-0.
Alisema aliamua kuingia kugombea ili apate nafasi ya kuongoza kutokana na kuona kwamba mambo yalikuwa yamevurugika, wanachama hawakuwa wakiuamini uongozi na hofu iliingia.
Baada ya kushinda uchaguzi alisema kitu cha kwanza kilikuwa ni kurudisha imani kwa mashabiki wa Yanga na alifanikiwa.
Alitaka wajiamini tena na kuamini kwamba Yanga iliteleza tu na kufungwa mabao yale matano na inaweza kurejea katika hadhi yake.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic